Thursday, October 9, 2014

CHEKA NASI

..BUBU MMOJA ALIULIZWA JINA LAKE. AKAJIBU KWA ISHARA: AKASHIKA KOO NA MBOO. MKALIMANI AKASEMA "HUYU ANAITWA KO MBO". AKAULIZWA UNAKAA WAPI. BUBU AKAVUA NGUO NA KUONYESHA MKUNDU WAKE  MKALIMANI AKASEMA "HUYU ANAKAA HUKO KUNDUCHI". AKAULIZWA KWENU WANAONGEA LUGHA GANI.  BUBU AKASHIKA KISU NA AKAMSHIKA DADA MMOJA SEHEMU ZA SIRI,  DADA AKAWA MKALI NA KUTAKA KUPIGANA NA BUBU. MKALIMANI AKASEMA "HAPANA DADA HUYU ANA MAANA HUKO KWAO WANAONGEA KISU KUMA". CHEZEA BUBU WEWE!!

#######################

Mzee mmoja aliongozana na binti yake kwenda kwa mwanaume aliyempa mimba huku akitweta kwa hasira. Walipofika ilikua hivi: Mzee, wewe ndiye ulimpa mimba bint yangu?
KIJANA: Mzee ni kweli mimi nimempa mimba binti yako, ila akizaa dume nitakupa daladala kumi, sheli 3 na milioni 50 za mtaji. Akizaa jike, nitakupa supermarket 3, mashamba 6 na milioni 40.
BINTI AKADAKIA: Je mimba ikitoka?
MZEE: Nyamaza mshenz ww, si atakupa nyingine... N hatareee aisee.

Wednesday, October 8, 2014

SIMBA YAENDA KAMBI S.AFRICA KWAAJILI YA MAANDALIZI YA MECHI DHIDI YA YANGA

Kikosi cha Wekundu wa Msimbazi
kimebadili muelekeo na sasa
kinatarajia kuondoka nchini leo,
Jumatano kuelekea Afrika Kusini kwa
ajili ya kuweka kambi kujiandaa na
mechi ya mzunguko wa kwanza dhidi
ya watani wao jadi, Yanga
utakaochezwa Oktoba 18, mwaka huu
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Awali NIPASHE ilifahamishwa kwamba
Simba ingekwea pipa kuelekea
Muscat, Oman kwa ajili ya kambi
hiyo, lakini ghafla ikabadili muelekeo
huo.
Kikao cha Wajumbe wa Kamati ya
Mashindano kilichokutana juzi jioni
ndicho kilichofikia maamuzi hayo
baada ya kuwa na mapendekezo
mawili ya kuipeleka timu Oman au
Afrika Kusini kujifua.
Akizungumza na gazeti hili jana,
kiongozi mmoja wa klabu hiyo yenye
makao makuu mtaa wa Msimbazi,
Kariakoo jijini, alisema kuwa timu
hiyo itaweka kambi ya siku 10 katika
jiji la Johanesburg.
Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo
zinaeleza kuwa awamu ya kwanza ya
wachezaji wataondoka jijini leo jioni
na kundi la pili ambalo litakuwa na
wachezaji walioko katika kikosi cha
timu ya Taifa (Taifa Stars) kitaondoka
Jumapili usiku.
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba
huenda timu hiyo ikiwa Afrika Kusini
itacheza mechi moja ya kirafiki ya
kimataifa na klabu mojawapo
inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo na
taratibu za kupata mchezo huo
zimeshaanza.
"Timu itaondoka kesho (leo) jioni na
itarejea siku moja kabla ya mechi,"
alisema kiongozi huyo.
Alisema kuwa wanaamini kambi hiyo
itasaidia kuimarisha kikosi chao na
sare walizopata hazijawakatisha
tamaa.
Simba ina pointi tatu baada ya kupata
sare tatu mfululizo katika mechi zake
zilizotangulia dhidi ya Coastal Union
ya Tanga, Polisi Morogoro na Stand
United kutoka mkoani Shinyanga.
Yanga yenyewe itashuka dimbani
ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa
mabao 2-1 walioupata dhidi ya JKT
Ruvu ya Pwani na Prisons, lakini
wakiwa na doa la kichapo cha 2-0
kutoka kwa Mtibwa Sugar ya
Manungu, mkoani Morogoro katika
mechi ya ufunguzi wa ligi hiyo.
Awali mechi hiyo ya watani wa jadi
ilipangwa kufanyika Oktoba 12 lakini
ikasogezwa mbele na Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) ili kupisha
maandalizi ya timu ya Taifa (Taifa
Stars) kuikabili Benin katika mchezo
wa kirafiki wa kimataifa.

MAANDALIZI YA KUKABIDHI KATIKA MPYA KWA KIKWETE YAKAMILIKA

Wakati Maandalizi ya kuwakabidhi
Rais Jakaya Kikwete na Rais wa
Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein
Katiba inayopendekezwa, leo mjini
Dodoma, vyama vinavyounda Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),
vimesema havitashiriki tukio hilo kwa
madai kuwa maoni ya wananchi
yamechakachuliwa.
Vyama hivyo ni Chadema, CUF na
NCCR-Mageuzi.Katibu Mkuu wa
Chadema, Dk. Willibrod Slaa
(pichani), alisema wao hawatashiriki
kwa madai ya kwamba mawazo ya
wananchi yaliyokuwamo kwenye
Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na
iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, yalichakachuliwa.
“Sisi Chadema hatutashiriki kwa
sababu mawazo ya wananchi
yamechakachuliwa. Makundi
mbalimbali kama vile ya wakulima,
wafugaji yamekuwa yakichukuliwa
kwa makundi na kuambiwa
wakubaliane na katiba
iliyopendekezwa. Wananchi hao
hawana uelewa wa kutosha, hivyo
wanaamini kiongozi wao
anachokisema hata kama ni uongo.
Tunafanya usanii, sisi Chadema
hatuko tayari kushiriki usanii huo.”
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James
Mbatia, alisema hawezi kusema
chochote kuhusu makabidhiano hayo,
kwa kuwa hawajapewa mwaliko
wowote.
Kwa mujibu wa Mbatia, ofisi yake
ingepewa mwaliko wa kuhudhuria
tukio hilo, angeweza kujua kitu gani
kilichomo kwenye barua na hivyo
kuweza kusema chochote kuhusu
tukio hilo linalotarajia kufanyika leo
katika Uwanja wa Jamhuri, mjini
Dodoma.
“Hatujaalikwa. Mimi kama mwenyekiti
wa chama, ningepata mwaliko,
ningeona maudhui na kujua la
kusema. Sasa nitawezaje kusema,
ikiwa hatujaalikwa na maudhui
siyajui?” Alihoji Mbatia.
Hata hivyo, alisema, wao hawawezi
kujihusisha kwenye tukio ambalo
halina maridhiano kwa madai ya
kwamba, dola inaendeshwa kwa
maridhiano huku akionyesha
kusikitishwa na hatua iliyofikiwa na
BMK ya kuwatukana viongozi wa dini
wakati zoezi la mwisho la kuipigia
kura katiba hiyo iliyopendekezwa na
bunge hilo wiki iliyopita.
“Nchi bado haijakaa vizuri, nami
siwezi kushiriki kupokea katiba
inayounganisha nchi ya namna hiyo.
Hivyo namshauri Rais, leo
azungumze namna ya kuliunganisha
taifa.”
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CUF,
Joran Bashange, alisema, wao
walishakataa baada ya kuona
mchakato wa upatikanaji wa katiba
mpya ulikuwa unaenda kinyume na
matakwa ya wananchi.
“Wamepanga utaratibu wao, sisi
tutakubalianaje? Sisi tulikataa kwa
sababu tuliona mchakato ulikuwa
unaenda kinyume cha matakwa ya
wananchi. Hivyo hatuwezi kwenda
kubariki uharamia.”
Naye mjumbe wa iliyokuwa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba (TMK), Prof.
Mwesiga Baregu, alishauri tukio la
kukabidhi katiba inayopendekezwa,
lifanyike kimya kimya.
“Ninasikia kuwa kuna maandalizi ya
sherehe za kukabidhi Katiba hiyo
yanayoambatana na nyimbo mpya
zilizoandaliwa kwa ajili ya kuimbwa
kwenye tukio...mimi nashauri
makabidhiano yafanyike kimya
kimya,” alisema Prof. Baregu na
kuongeza:
“Ninashauri hivyo kwa sababu kwa
sasa inaonekana kwamba hatua ya
kupitisha katiba hiyo imekuwa kama
ni ushindi kwa wale walioipitisha na
kumbe sivyo.”
“Watanzania wanataka Katiba
inayowaunganisha na siyo
inayowatengenisha, hivyo kuruhusu
sherehe kwenye makabidhiano hayo
ni kuendeleza msuguano miongoni
mwa makundi yanayopingana kuhusu
katiba hiyo," alisema.
Prof. Baregu alisema kuwa cha msingi
ambacho kilikuwa kinatakiwa ni
maridhiano ili kupata kile wananchi
wanakihitaji, hivyo kushangilia ama
kusherehekea bila kuwa na
maridhiano ni kuongeza mpasuko
kwenye jamii.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk.
Rehema Nchimbi, alisema hadi jana
mchana, tayari mazingira ya uwanja
wa Jamhuri yalikuwa tayari
yameshaandaliwa.
Hata hivyo alipoombwa kutaja majina
ya viongozi wakuu waliothibitisha
kuhudhuria sherehe hizo, Dk. Nchimbi
alisema orodha ipo kwa Katibu wa
BMK kwani wao ndiyo wanaoratibu
shughuli hiyo.
Kwa mujibu wa tarifa za awali
zilizopatikana kutoka kwa ofisa
mmoja wa serikali, sherehe hizo
zinatarajiwa kuhuduriwa na wageni
takribani 3,000.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa,
David Misime, alisema
wamejiimarisha kiulinzi na kwamba
kutakuwa na doria katika maeneo
mbalimbali yakiwamo ya mjini.
“Tunafuatilia taarifa mbalimbali kwa
ajili ya kuimarisha usalama, vijana wa
kufanya doria kwa miguu, farasi,
pikipiki na magari wapo muda wote
kuanzia sasa,” alisema Kamishna
Misime.

Saturday, October 4, 2014

AUTHOR SOPHIE KINSELA: 10 tips of being a best-selling author

Here are Kinsella's top 10 tips for
being a bestselling author.
1. Always carry a notebook
Carry a notebook everywhere and
write down everything that springs to
mind, even if it doesn't seem relevant
at the time. You can do a lot with a
passing thought or a little bit of
overheard dialogue.
Get into the habit of looking at life
like a writer and writing it all down.
Don't worry about what "it" is going
to be yet, just write it down as a
habit. Because then, when you do
have your big idea and want to write
a book, you'll already be used to that
process and have material to work
with.
2. Think "what if" and read
Start to see the world in a "what if"
way and keep your possibilities for a
story. Teach yourself to take a tiny
little nugget of substance and
extrapolate and tease it out into
something else, have fun with it and
see the potential.
It can seem tiny and insignificant but
if you can sense the grain of a story
there and keep your mind open to
those possibilities, you will
constantly come up with new ideas.
Reading is vital if you want to be a
writer, it's essential. I've been a
bookworm ever since I was a child, I
was the type who would read a cereal
packet over and over rather than
make conversation at breakfast!
3. Write the book that you want to
read.
People often think that they should
write to please someone else,
whether it is to please the audience,
or critics, or a readership. My instinct
has always said that you can't
second guess anybody else.
'What you have to do is find your
story and find your voice,' says
Sophie Kinsella
What you can do, is think if you were
a reader, what would you want to
read? One way to visualise that is to
go into a shop and imagine the book
that would make you want to grab it
off the shelf.
The chances are that if you would
grab it off the shelf and be excited to
read it. then other people would too.
So always start with yourself, write
something that will please you.
4. Don't talk about what you're
writing
I am very secretive when I'm writing a
new book. I think that writers are very
fragile, they're like butterflies or
perhaps moths; they can be easily
crumpled. If you're very sensitive,
which I am, it only takes a raised
eyebrow or a chance remark about an
idea for you to lose confidence in it.
I think it's much better to let these
things gestate in private, that way
you can be free to try stuff out
without any fear of being judged or
worrying whether it might not work.
The minute you put it out there and
ask for opinions from other people, it
will just get in the way of your
creativity.
The only person I let read my work
when I'm writing is my husband and
we've had this arrangement long
enough that he knows what not to
say! I think a work in progress is a
very precious and nebulous thing and
it can be easily destroyed so protect
it!
5. Forget about genre to find your
voice
I think that one of the hardest things
as a writer is to find your voice. See
what you enjoy writing, because let's
face it, you're going to be spending a
long time in this zone, it had better
be something you enjoy and
something which you can do.
Don't be afraid of a few false starts. I
once tried to write a thriller and I
remember my agent saying that the
plot was ok but that all the characters
were far too nice. I'd written about all
these nice middle class people
walking around killing each other!
Don't sit there thinking what genre
should I write in, perhaps you'll
invent a whole new one! Instead,
start off by thinking I'm going to write
a story and wait for other people to
put it in a genre. What you have to do
is find your story and find your voice.
6. Just get to the end
It's the hardest thing and it's the
most important thing because so
many of us have ideas for books. The
first stage is actually write it instead
of just talking about it, and the next
stage is to keep going until you get
to the end.
Everybody, no matter who they are
gets to the middle of a book and
thinks crikey, I've had enough of this.
You get bored with your story and
your characters, you hate them all,
you can't think why you started this
wretched story in the first place.
The truth is, every book is hard to
write, everybody reaches a wall,
whether it is a plot hole or a scene
that you can't get past. So you've
just got to get to the end. Even if it's
not the greatest draft, if it needs
rewriting fine, at least you have a
book to rewrite.
7. Walk and drink cocktails!
Everybody gets stuck. I find cocktails
very helpful! And that's the truth, if I
get stuck, I'll go out with my
husband and we'll order cocktails
and talk while we drink them. By the
end of the evening, we've always
ironed out the knot.
I find it loosens you up and also it
turns it into a fun project, there's
nothing worse than sitting grimly
staring at a screen, you must get out.
The other thing to do is go for a
walk, walking seems to free up the
cogs of the brain like nothing else.
You can sit at your desk for two
hours, feeling wretched because you
can't find the solution, then you give
up and go for a walk and it comes to
you straight away.
8. Plan your books
For me, the planning stage is vital
and it takes months, if not years.
When I'm writing a book, I do it in my
office, but when I'm planning a book I
like going and sitting in coffee shops.
I like the buzz and I like being
surrounded by people, but remaining
anonymous.
I write my plot points on file cards
and Blu Tac them to the wall. Then I
stand back and look at the terrain of
the story and decide whether I like it
and if not I can just move them
around. I find that very satisfying -
it's a bit like doing a crossword
puzzle!
The truth is you can plan and plan
but during the story, something will
change, that's just the way it is. But I
find starting off with structure and a
beginning, a middle and an end is
vital.
9. Get a great agent and consider a
pseudonym
I think I've written 20 books in total
now and I've always had the same
agent. Having an agent, for me is the
best thing I've ever done, because
she's guided me, she's been a friend,
she's dealt with all the business side
of what I do and I wouldn't have
known where to start without her.
There are lots of advantages to
having a pseudonym. It gives you a
bit of privacy so you can have an
official name and a home name. And I
don't think there are many careers
where you can just completely
reinvent yourself every so often - it's
wonderful.
10. Write the next you
Everyone has got a story to tell and
everyone can learn and improve their
writing. There are some elements of
writing which can definitely be
taught, a sort of craft and you should
always try to learn and improve. I am
still learning with every book.
I don't see why anybody shouldn't
write a book. There is nobody who is
not interesting in this world, so why
shouldn't they tell their story?
You write what you write. You can't
decide to write a certain book, I
believe your writing finds you. So
don't go thinking, I'm going to write
the next Da Vinci Code or the next
Stephen King. Write the next you.
You are going to be the next big
thing!

RAIS MWANZILISHI WA HAITI (JEAN-CLAUDE

Duvalier was just 19 when in 1971 he
inherited the title of "president-for-
life" from his father, the notorious
Francois "Papa Doc" Duvalier.
He was accused of corruption, human
rights abuses and repression in his
rule, which ended in a 1986 uprising.
After years of exile in France, he
returned to Haiti in 2011.
His death was announced by Haiti's
health minister, and the ex-leader's
attorney Reynold Georges confirmed
he died at home on Saturday.
Lavish wedding
At the time of his swearing in, Jean-
Claude Duvalier was the youngest
president in the world.
Initially it seemed that there could be
a significant move away from his
father's harsh regime, underpinned as
it was by Haiti's notorious secret
police, the Tontons Macoutes, says
BBC world affairs correspondent Mike
Wooldridge.
For some time, Jean-Claude Duvalier
was the youngest president in the
world
He moved closer to the Americans,
from whom his father had been
estranged. US businesses moved in
and he allowed limited press freedom.
But Jean-Claude Duvalier lived
lavishly. His state-sponsored
wedding reportedly cost $5m in 1980,
while most of the people in his
ravaged nation endured the worst
poverty in the Western hemisphere.
Repression continued, too, and amid
massive unrest in 1986 he fled to
France.
Human rights groups say thousands
of political prisoners were tortured or
killed under his rule, and he was
accused of massive corruption.
He described his return to Haiti - a
year after it was devastated by a
major earthquake, as a gesture of
solidarity to the nation.
His unexpected return to Haiti saw
him arrested and charged, but the
case against him stalled
But he was arrested and charged, and
although released he finally appeared
in court in February 2013, where in an
emotionally-charged hearing in front
of some of his alleged victims, he
denied responsibility for abuses
carried out during his time as
president.
Judges ruled he could face crimes
against humanity charges, but the
case had stalled some time before he
died.
Jean-Claude 'Baby Doc' Duvalier
Jean-Claude Duvalier, pictured here
in 1980, ruled Haiti with an iron fist
for 15 years
Took over presidency aged just 19
when his father, Haiti's
authoritarian leader Francois "Papa
Doc" Duvalier, died in 1971
Called himself "president-for-life"
and ruled with an iron fist, aided
by a brutal private militia known
as the Tontons Macoutes
Accused of corruption and human
rights abuses that prompted more
than 100,000 Haitians to flee the
country during his presidency
Ruled for 15 years before outbreak
of popular protests led him to flee
to France in 1986
Asked Haitian people for
forgiveness for "errors" made
during his rule in a 2007 radio
interview
Returned to Haiti in 2011 as it was
supposed to hold run-off elections
to choose successor to outgoing
President Rene Preval

PHIL AAHIDI MABADILIKO YA SIMBA

Simba itakayoingia Uwanja wa Taifa
kucheza mechi yake ya tatu ya ligi
kuu ya Bara dhidi ya Stend United leo
baada ya sare mbili mfululizo itakuwa
kama mpya, kocha Patrick Phiri
amesema.
Akizungumza na gazeti hili jana, Phiri
alisema katika mchezo wa leo
atafanya mabadiliko kwenye kikosi
chake ili kuweka uwiano kati ya ulinzi
na mashambulizi kwenye kikosi.
Phiri alisema "Tumechoshwa na
matokeo ya sare" na kwamba
amefanya marekebisho kwenye kikosi.
"Kama utakuwepo uwanjani utaona.
Lengo ni kuiimarisha timu ili kuleta
ushindi."
Kocha huyo Mzambia alisema ushindi
kwenye mchezo wa leo utawarudisha
wachezaji wake 'kwenye njia' baada
ya sare za nyumbani za 2-2 dhidi ya
Coastal Union na 1-1 dhidi ya Polisi
Morogoro.
"Baada ya mchezo dhidi ya Stand
United tutakutana na wapinzani wetu
(Yanga)... nimewaambia wachezaji
tunahitaji ushindi kabla hatujakutana
nao."
Simba ambayo inapewa nafasi kubwa
ya kufanya vizuri msimu baada ya
kumridisha Phiri aliyeipa ubingwa bila
kupoteza mechi mwaka 2010, ipo
pointi nne nyuma ya timu mbili
viongozi mabingwa watetezi Azam na
Mtibwa Sugar.
Aidha, aliwataka mashabiki wa timu
hiyo kutokata tamaa na timu yao
kwani Simba ni timu nzuri na makosa
ya yanayoonekana yanarekebishika na
kuomba kupewa muda kwa wachezaji
wake.

KLA

Klabu za ligi kuu ya Bara zinakusudia
kupeleka katika mkutano mkuu wa
shirikisho la soka (TFF), hoja ya
kutokuwa na imani na rais Jamal
Malinzi.
Klabu hizo, kupitia kwa wakili Dk.
Damas Ndumbaro, zilisema jijini jana
kwamba zitakusanya theluthi mbili ya
kura za wanachama wa TFF ili
kuitisha mkutano mkuu na kupeleka
hoja mbili, ikiwemo hiyo ya
pendekezo la kumng'oa rais
madarakani.
Mkutano mkuu wa TFF una madaraka
ya kumuondoa rais madarakani
kikatiba.
Mbali na hoja ya kutokuwa na imani
na Malinzi, pia klabu zitawasilisha
hoja ya kutaka kufanyike ukaguzi wa
hesabu za fedha za TFF zinazotolewa
na wadhamini wa ligi kuu tangu
kuingia madarakani kwa Malinzi,
Ndumbaro alisema.
Hatua hizo zinafuata baada ya klabu
hizo kuiagiza Bodi ya Ligi Kuu (TPLB)
kutokubali makato ya ziada ya
asilimia tano ya fedha za wadhamini.
TFF imedai inataka kupeleka fedha
hizo kwenye mfuko wa TFF wa
maendeleo ya soka ya vijana.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini jana, Ndumbaro alisema klabu
hazikubali makato ambayo TFF
imeagiza.
"TFF inapata fedha nyingi zaidi ya
vilabu kwa mwaka," alisema
Ndumbaro. "Kwa mfano katika
udhamini wa Azam TFF peke yake
inaingiza zaidi ya milioni 400 huku
vilabu vikiingiza milioni 331.
"Lakini bado katika fedha hizo ndogo
wanazopata vilabu TFF wanataka
kuzikata... kimsingi wateja wangu
(klabu) hawakubali na wanalipinga
suala hili."
Aidha, Ndumbaro alisema kukatwa
Sh. 1000 kabla ya kodi katika mapato
ya kila tiketi iliyotumika kuingia
uwanjani ni hujuma inayofanywa na
TFF kwa serikali, klabu na chama cha
mapinduzi kinachomiliki viwanja vingi
vya soka nchini.
Alisema serikali inadhulumiwa kwa
kodi kutolipwa kwa Mamlaka ya
Mapato (TRA) na hivyo kurudisha
nyuma maendeleo ya nchi na ya klabu
za ligi kuu.
Ndumbaro alisema kugomea kucheza
ligi kuu ni moja ya njia ambazo klabu
zimepanga endapo muafaka
hautapatikana.
Ndumbaro alisema klabu zipo tayari
kukutana na TFF kwa muzungumzo.

BUNGE LA KATIBA MSHTUKO

Uamuzi wa baadhi ya wajumbe wa
Bunge Maalum la Katiba kupiga kura
ya hapana kwa ibara zote za rasimu
mpya ya katiba inayopendekezwa
imeibua mkanganyiko na sasa Kamati
ya Mashauriano imeundwa kukutana
na waliopiga kura hizo.
Juzi wajumbe walianza kupiga kura
kupitisha sura na ibara moja baada ya
nyingine, kwa wazi au siri, huku
wengi wakisema kuwa wanaunga
mkono, lakini pia wakiwamo
wachache waliosema hapana kwa
sura zote 10 na ibara zote kuanzia ya
kwanza hadi ya 157.
Jana Mwenyekiti wa Bunge hilo,
alitaja kamati hiyo kuwa inaundwa na
Makamu Mwenyekiti wa BMK, Samiah
Hassan Suluhu, Rashid Mtuta, Shamsi
Vuai Nahodha, Omari Yusuph Mzee,
Andrew Chenge, Asha-Rose Migiro,
Dk. Francis Michael, Brigedia Jenerali
Mstaafu Hassan Ngwilizi na
Mohammed Aboud.
Bunge hilo limefikia hatua ya kupiga
kura ambayo ni nyeti zaidi kwani
zitahitajika theluthi mbili kutoka kila
upande wa Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania ili kufanikisha upitishwaji
wa rasimu hiyo.
Kulingana na mahudhurio
yaliyokuwako juzi kabla ya kuanza
kwa kazi ya upigaji kura, wajumbe
kutoka Tanzania Bara walikuwa 295,
huku kutoka Zanzibar wakiwa ni 142.
Kulingana na hesabu hizo, zitahitajika
kura 140 kutoka Zanzibar na kura 280
kutoka Tanzania Bara ili kupitisha
ibara hizo.
Kwa mahudhurio ya juzi, Zanzibar
ilikuwa na wajumbe wawili zaidi ya
idadi ya theluthi mbili inayohitajika
huku bara kukiwa na wajumbe 15
zaidi ya theluthi mbili ya kura
zinazohitajika.
Hata hivyo, siyo wajumbe wote
walipiga kura za ndiyo na hata
waliopiga za ndiyo wapo waliokataa
baadhi ya ibara. Walikuwapo
waliokataa huku wengine wakipiga
kura za siri, ambazo haijulikani
waliamua nini.
Hali hii inatafsiriwa kama juhudi za
kusaka theluthi mbili ya kura za
wajumbe kutoka Zanzibar, kwa ajili
yakupitisha Rasimu hiyo.
Mwenyekiti wa Bunge hilo juzi
alisema kwa kuzingatia idadi ya
wabunge waliokuwamo bungeni kwa
wakati huo, upande wa Zanzibar
ulikuwa na wajumbe wawili tu
wanaozidi idadi ya inayotakiwa
kupata theluthi mbili, hivyo
akawaomba wote wapige kura ya
ndiyo ili kutimiza matakwa ya
kisheria.
Hata hivyo, zoezi la kupiga kura
lilipoanza, wabunge saba kutoka
Zanzibar walipiga kura ya wazi ya
hapana, huku wengine zaidi ya 20
wakipiga kura ya siri.
Hali hiyo imelifanya BMK kushtuka
kutokana na kuwapo kwa dalili ya
kukosekana kwa theluthi mbili ya kura
za ndiyo kutoka Zanzibar, hivyo
kuufanya uongozi wa Bunge hilo
kuanza kuhangaika kuweka ‘mambo
sawa’.
Kamati ya mashauriano iliundwa kwa
ajili ya kuwasikiliza wajumbe
waliopiga kura ya hapana dhidi ya
rasimu nzima.
Akizungumza saa 5:50 wakati wa
kipindi cha Matangazo jana,
Mwenyekiti wa BMK, alisema kuwa
uongozi umeshtushwa na uamuzi wa
wajumbe hao kupiga kura ya hapana
kwa rasimu nzima huku wakiwa
wametumia muda mwingi kuijadili
jambo ambalo siyo la kawaida.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo,
ameamua kuunda Kamati ya
Mashauriano kwa ajili ya kuwasikiliza,
huku akidai kuwa wajumbe wawili
kati ya waliopiga kura ya kuipinga
rasimu hiyo waliomba kusikilizwa.
Alisema kuwa kanuni ya 54, kanuni
ndogo ya nne inasema kwamba
‘Mwenyekiti baada ya kushauriana na
Kamati ya Uongozi anaweza kuunda
kamati ya mashauriano pale anapoona
linajitokeza suala linalohitaji
mashauriano’.
“Nina suala mbele yangu linalohitaji
mashauriano kutokana na baadhi ya
wabunge wenzetu ambao jana (juzi)
walipiga kura ya hapana kwa ibara
zote kitu ambacho si cha kawaida
kwa sababu haiwezekani kuwa hivyo,”
alisema Mwenyekiti huyo.
“Tunaomba Kamati hii ifanye kazi leo
(jana) na sisi tutapokea matokeo
baadaye na kuyaleta ndani ya Bunge
hili kwa wakati unaofaa,” alieleza
Mwenyekiti huyo.
Alisema kuwa ingawa wajumbe wawili
kati ya waliokataa Rasimu hiyo juzi
walimuomba kusikilizwa pia milango
ya kamati hiyo itakuwa wazi hata kwa
wajumbe wengine ambao hawajaomba
ili ieleweke kwanini wakae wakati
walikaa kipindi chote bungeni kisha
waikatae rasimu yote.
Baadhi ya wajumbe wa BMK
waliozungumza na NIPASHE jana
mjini Dodoma walielezea
kutoridhishwa na hatua hiyo,
wakiamini kanuni ililenga kuundwa
kwa kamati wakati wa vipindi vingine
vya uhai wa BMK, lakini siyo katika
kipindi hiki cha upigaji kura.
Walisema kuwa kitendo cha kuundwa
kamati hiyo katika kipindi cha kupiga
kura, wanakitafsiri kuwa ni kuingilia
uhuru wao wa kufanya maamuzi.
Dk. Alley Nassoro, alisema yeye siyo
miongoni mwa walioelezwa na
Mwenyekiti wa BMK, kuwa wameomba
kusikilizwa na kwamba hajutii kupiga
kura ya hapana kwa rasimu yote kwa
sababu ana amini ndiyo msimamo
halisi alionao juu ya kazi yote
aliyofanya tangu BMK lilipoanza.
“Sababu zangu kuu ni mbili tu
ambazo zimesababisha nipige kura ya
hapana, ya kwanza ni imani na uzawa
wangu; nikimaanisha dini ya kiislamu
kunyimwa haki ya Mahakama ya Kadhi
kutambuliwa na kuheshimiwa kikatiba
lakini ya pili ni maslahi ya nchi yangu
Zanzibar, kutozingatiwa na Katiba hii
kwa kiwango cha kukidhi matarajio
yangu,” alisema Dk. Alley.
Alisema hata ahadi iliyotolewa
bungeni na Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, wakati wa mijadala ya
kuboresha Rasimu hiyo ya Katiba
inayopendekezwa, kwamba Mahakama
ya Kadhi itatungiwa sheria haafikiani
nayo kwa sababu siyo mara ya
kwanza kwa serikali kutoa ahadi juu
ya jambo hilo.
Alisema kwamba hata ikitungwa
sheria ya aina hiyo, utekelezaji wake
unaweza usifanyike kwa sababu
utategemea zaidi uongozi
utakaokuwa madarakani tofauti na
kama haki hiyo ingewekwa kwenye
Katiba ambayo ndiyo sheria mama.
“Hii Katiba inayopendekezwa kwa
jinsi ilivyowekwa ni dhahiri hata
kama ikitungwa sheria ya kuanzisha
Mahakama ya Kadhi, utekelezaji wake
utakuwa mgumu kwa sababu baadhi
ya watu wanachukulia baadhi ya
masharti katika imani yetu kuwa ni
yenye chembe za kibaguzi hususan
katika umiliki wa mali baina ya
mwanamke na mwanaume,” alieleza
Dk. Aley.
Suala la kupata theluthi mbili ya kura
za upande wa Zanzibar linakuwa tete
kutokana na wabunge wa Chama cha
Wananchi, CUF pamoja na wale wa
kundi la 201 ambao waliungana na
kundi la Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa) na kuondoka
bungeni, hali inayosababisha idadi ya
wajumbe waliobaki kupata wakati
mugumu kutimiza matakwa ya
kisheria ya kuhakikisha Rasimu hiyo
inapitishwa na theluthi mbili ya kura
za wajumbe wote kutoka katika kila
nchi washirika.
Imeandaliwa na Emmanuel Lengwa,
Editha Majura, John Ngunge na
Jacqueline Massano, Dodoma.

KESI YA MWANAFUNZI ALIYELAWITIWA YAFUTWA

Kesi ya mwanafunzi wa darasa la tatu
(jina linahifadhiwa) katika Shule ya
Msingi Ukombozi iliyofunguliwa
katika Kituo cha Polisi cha Urafiki,
jijini Dar es Salaam baada ya kudaiwa
kulawitiwa imefutwa.
Kesi hiyo ambayo ilifunguliwa
Septemba 15, mwaka huu kituoni
hapo, ikimkabili mtuhumiwa
aliyetajwa kwa jina moja la Enock,
imefutwa jana na mtu huyo kuachiwa
huru kwa madai kuwa, imekosa
ushahidi.
Mama wa mtoto huyo (jina
linahifadhiwa), aliliambia gazeti hili
kuwa, mpelelezi wa kesi hiyo
aliyemtaja kwa jina moja la Suzana
aliiambia familia hiyo kuwa, baada ya
jalada la kesi kupelekwa kwa
mwanasheria na kulipitia, alikosa
ushahidi wa kulipeleka shauri hilo
mahakamani.
Alisema baada ya kuripoti tukio hilo
kituoni hapo alipewa RB/
Urafiki/7627/2014.
Aidha, mama huyo alisema mjomba
wa mtoto alipofuatilia kesi hiyo jana
kituoni hapo alirudi na majibu kuwa
imefutwa.
Alisema kuwa baada ya kukutana na
mpelelezi wa kesi hiyo, alimweleza
kuwa jalada la kesi limerudi kutoka
kwa mwanasheria na mtuhumiwa
anaachiwa huru kutokana na
kukosekana ushahidi.
Alisema baada ya maelezo ya
mpelelezi, aliomba kuonana na Mkuu
wa Kituo hicho, ambaye naye
alimweleza kuwa, majibu ya daktari
yalionyesha hajalawitiwa.
Pia alisema mkuu huyo wa kituo
alimweleza kuwa alichokieleza mtoto
kuhusu mazingira ya nyumbani kwa
mtuhumiwa yalikutwa tofauti.
Siku ya tukio mtuhumiwa huyo
alikamatwa baada ya mama
kuambatana mtoto wake siku ambayo
kijana huyo alikuwa na miadi ya
kukutana na mwanafunzi huyo.
Kabla ya kukamatwa kwake, kijana
huyo ilidaiwa alishamfanyia vitendo
hivyo mtoto huyo zaidi ya mara moja
na alikuwa akimpa fedha kati ya Sh.
2000 na Sh. 7000 lakini siku ya
kukamatwa alimpa Sh. 200.
Awali, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,
Biamina Swai, aliliambia gazeti hili
kuwa, kwa mwaka huu jumla ya
matukio manne ya watoto kufanyiwa
vitendo hivyo yalitokea lakini hilo
moja ndilo mtuhumiwa wake
alikamatwa baada ya kushirikiana na
mzazi wake.
Alisema matukio mengine baada ya
wazazi kupewa taarifa za ulawiti wa
watoto wao, pindi waendapo mitaani
huvujisha siri na kusababisha
wahusika kukimbia.

WANAUME 400,0

Serikali imesema jumla ya wanaume
400,000 kutoka mikoa minne nchini,
wamefanyiwa tohara katika kampeni
iliyomalizika hivi karibuni.
Katika hotuba ya Waziri wa Afya na
Ustawi wa jamii, Dk, Seif Tashid,
iliyosomwa na Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo, John Michael, wakati wa
ufungaji wa kampeni hiyo jijini Dar es
Salaam jana, alisema mikoa
iliyohusika na kampeni hiyo ni Iringa,
Njombe na Tabora.
Zoezi la kuwafanyia tohara wanaume
lililofahamika kama `tohara ya
kitabibu ya wanaume’ (VMMC)
iliendeshwa kwa ushirikiano kati ya
Serikali ya Tanzania, Marekani na
Shirika la Jhpiego.
Alisema zoezi hilo limesaidia
kupunguza kasi ya maambukizi ya
virusi vinavyosababisha Ukimwi
(VVU) nchini, kitu kinachoonyesha
lengo la kufikia maambukizi ya
asilimia 0.16 hadi mwaka 2018
linaweza kufikiwa.
Baada ya kuonekana kwa mafanikio
hayo, mikoa mingine 12 ambayo
wanaume wake wapo nyuma katika
kufanyiwa tohara imeteuliwa
kuendelea na zoezi hilo.
Kiasi cha Dola za Marekani Milioni 34
zimetengwa kwa ajili ya kuendesha
kampeni hiyo.
Dk. Rashid alisema lengo ni kuwafikia
watu milioni 2.1 walio na umri kati ya
miaka 10 hadi 34 kufikia mwaka 2017.
Awali, Naibu Mkurugenzi wa Shirika
la Misaada la Marekani nchini (USAID)
, Timoth Donny, alisema katika tafiti
mbalimbali zinaonyesha kwamba
wanaume waliofanyiwa tohara
wanaondokana na hatari ya
kuambukizwa VVU kwa silimia 60,
hivyo kuna wajibu wa kuhakikisha
elimu inatolewa sehemu zote nchini.
Alisema nchi yake ipo tayari kusaidia
katika kupambana na hali hiyo katika
nyanja ya kujengea uwezo wa
mafunzo na vitendea kazi kwa watoaji
huduma.
Naibu Rais wa Shirika la Jhpiego,
Alain Damiba, pamoja na kuishukuru
serikali kwa kutoa msaada mkubwa
katika kutekeleza mkakati huo, shirika
lake kwa kushirikiana na washirika
mbalimbali litaendelea kufanya kazi
kwa ajili ya kuboresha afya za
wananchi na kuongeza kasi ya
maendeleo.

Friday, October 3, 2014

WAKAZI JIJINI MBEYA WAHAURIWA KUTUMIA VIZURI FURSA

Mlezi na mshauri wa asasi ndogo
ndogo la kifedha (Vicoba) mkoani
Mbeya, Dk. Stephen Mwakajumilo,
amewataka wananchi wa mkoa huo
kutumia fursa mbalimbali
zinazowazunguka ili kujitegemea
kiuchumi na kuacha kutegemea
wafadhili.
Dk. Mwakajumilo aliyasema hayo
alipokuwa akitoa elimu ya ujasiriamali
kwa waumini wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania (KKKT) katika mtaa
wa Lwambi, Usharika wa Itete
Halmashauri ya Busokelo wilayani
hapa.
Dk. Mwakajumilo ambaye ni pia
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Teofilo
Kisanji (Teku) cha jijini Mbeya,
alisema wilaya hiyo ni miongoni mwa
wilaya zenye utajiri mkubwa ambao
kama wananchi watautumia vizuri,
watakuwa na fursa nzuri ya kusukuma
gurudumu la maendeleo katika
maeneo yao.
“Nimeelezwa kuna vijana kadhaa
ambao wamemaliza vyuo vikuu kwa
taaluma mbalimbali hapa usharikani,
hakikisheni mnawatumia vijana hao
vyema kwa kuwapeni mbinu za
kufanya katika kutumia vizuri
rasilimali zilizopo ndani ya
halmashauri hii kwa manufaa ya jamii
hii na taifa kwa ujumla,” alisema.
Alieleza kuwa huu siyo muda wa
kuendelea kutegemea wafadhili katika
kuchangia shughuli za kimaendeleo,
wakati wananchi hao wana rasilimali
za misitu na ardhi ambayo ina rutuba
ya kutosha kwa kilimo cha mazao na
nyingine nyingi, hivyo kinachohitajika
ni elimu tu na kukubali kujitoa
kutumia fursa hizo.
“Mfano mzuri ni misitu tuliyonao hapa
kwetu tukiamua kwa dhati
kutengeneza mizinga ya nyuki kadhaa
katika usharika huu, nina hakika
tutaondokana kabisa na suala la
harambee za kila mara kuita watu
kutuchangia kwani tutapata fedha
nyingi ndani ya muda mfupi na
kutimiza malengo yetu,” alisema Dk
Mwakajumilo.
Aidha, alitoa mizinga mitatu na fedha
taslim Shilingi milioni moja kwa ajili
ya kuchonga mizinga mingine ili
kuwahamasisha waumini hao kuanza
rasmi shughuli ya ufugaji wa nyuki
huku akiahidi kupeleka mtaalam wa
nyuki kutoa elimu juu ya utunzaji na
uvunaji bora wa asali.

WATANZANIA WANG'ARA KATIKA CHAGUO LA VIONGOZI WACHUMI WA KESHO AFRI

Watanzania watano wamechaguliwa
kuingia katika orodha ya viongozi
wachumi wa kesho 100 akiwemo
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
Mohammed Enterprises Tanzania
Limited (MetL), Mohammed Dewji.
Dewji ambaye pia ni Mbunge wa
Singida Mjini, alishika nafasi ya pili
kupitia utafiti wa kila mwaka
uliofanywa na Taasisi ya Choiseul ya
Ufaransa inayojishughulisha na
uchambuzi wa masuala ya kisiasa,
kiuchumi na utamaduni kimataifa.
Watanzania waliongia kwenye orodha
hiyo ma kampuni zao katika mabano
ni Genevieve Sangudi (Carley Group),
Elsie Kanza (Mkuu wa World
Economic Forum-Afrika), Patrick
Ngowi (Helvetic Group) na Denis
Dilllip ambaye ni Mwenyekiti wa
Canaco Tanzania.
Viongozi hao wamechaguliwa na
taasisi hiyo kwa kuangalia michango
ambayo wametoa katika mataifa yao
na Bara la Afrika kwa ujumla
yakiwamo kutoa ajira, uwekezaji wa
ndani na nje na uinuaji wa uchumi
kupitia biashara wanazofanya.
Katika orodha hiyo nafasi ya kwanza
imeshikwa na Igho Sanomi (Nigeria),
Mohamed Dewji ya pili, , Hisham El
Khazindar wa Misri (3), Isabel Dos
Santos wa Angola (4), Tidjane Deme
wa Senegal (5), Nomkhita Nqweni wa
Afrika Kusini (6), Mehdi Tazi wa
Morocco (7), Marlon Chigwende wa
Zimbabwe (8) huku nafasi tisa ikienda
kwa Ashish Thakkar wa Uganda
wakati ya kumi imechukuliwa na
Janine Diagouwodie wa (Ivory Coast)

TAMBWE AMTANGAZIA VITA KAVUMBAGU

Mfunguji bora wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu
uliopita, Amissi Tambwe amesema
ataanza 'kumshika' kinara wa mabao
kwa sasa Didier Kavumbagu kesho
wakati Simba itakapoivaa Stand
United kwenye Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaam.
Kavumbagu, mshambuliaji wa Azam
FC na timu ya taifa ya Burundi
'Entamba Murugamba', anaongoza
safu ya wafumani nyavu akiwa
amefunga mabao manne katika mechi
mbili za mwanzo ambazo mabingwa
hao watetezi walishinda 3-1 dhidi ya
Polisi Morogoro na 2-0 dhidi ya Ruvu
Shooting.
Hata hivyo, Tambwe katika mahojiano
na chanzo chetu  jijini Dar es Salaam jana
alisema zawadi ya mfungaji bora
itatua tena kwake na ataanza
kufukuzana na Kavumbagu katika
mechi ya kesho.
"Ninaona ametangulia tu, Simba kwa
sasa imeimarika, ninaamini tutaanza
kushinda kwa magoli mengi kuanzia
mechi inayokuja," alisema.
"Kikosi chetu kimeanza vibaya
kutokana na matatizo kidogo ambayo
tuliyazungumza kwenye kikao na
uongozi jana (juzi). Kazi yangu ni
kufunga, nitafunga zaidi yake,"
alisema zaidi Tambwe.
Raia huyo wa Burundi anayesifika kwa
kufumania nyavu, alijiunga na Simba
Agosti mwaka jana akitoka kuipa
ubingwa wa Kombe la Kagame klabu
ya Vital'O ya kwao, Burundi.

Tuesday, September 30, 2014

WAKAZI WA DAR WAPINGA MWEKEZAJI KUZIBA BARABARA

Wakazi wa eneo la Salasala wilayani
Kinondoni, Dar es Salaam wamepinga
uamuzi wa serikali kumpatia kibali
mwekezaji wa kampuni ya Mayfair na
kuziba barabara iliyokuwa ikitumika
kwa miongo miwili.
Mwenyekiti wa Kamati ya usimamizi
wa barabara hiyo, Seleman Magingi,
alisema hatua hiyo ya serikali
itawasababishi usumbufu wakazi
zaidi ya kaya 150 na viwanda.
Alisema mazingira ambayo kibali
hicho kimetolewa, yanaonyesha
viongozi wa Serikali ya Mtaa
kushawishiwa na rushwa.
“Kama mazingira hayo hayakuwa
rafiki mbona wananchi na wenye
viwanda hatukushirikishwa,ndiyo
maana mwekezaji huyo amepata
kiburi,” alisema Magingi.
Mmoja wa wakazi hao,Irene Shayo
alisema viongozi hao wanapaswa
kuangaliwa vizuri kupitia mwekezaji
huyo na kupoteza haki ya wananchi
kwa kununuliwa.
Alisema awali mwekezaji huyo
aliwarubuni kuwa atawaboreshea
miundombinu kama barabara,umeme
na maji wakati huduma hizo
zinapatikana kwa msaada wa viwanda
vilivyopo.
“Kufungwa kwa barabara hiyo
kutasitisha huduma zote za kijamii na
kiuchumi,”alisema.
Afisa Mtendaji wa Mtaa wa
Salasala,Ramadhan Ntai,eneo hilo
limefungwa baada ya mmiliki wa
kiwanja hichi kupata kibali kutoka
Wizara ya Ardhi,Nyumba na Makazi.
Alisema Wizara hiyo ilimtaka
Mwekezaji huyo kufanya marekebisho
ya ujenzi wa kubadilisha matumizi ya
kiwanja hicho ili barabara ipatikane.
Naye, Mmiliki wa Kampuni ya Mayfair
ambaye hakupenda jina lake
liandikwe alisema hayupo tayari
kuzungumza na vyombo vya habari.
“Siwezi kuongea na
waandishi,mtendaji anafahamu kila
kitu mtafuteni yeye,”alisema.
Diwani wa Kata ya Wazo, John Morro,
kupitia barua yake ya Oktoba mwaka
2013 yenye kumbukumbu namba
DSM/KN/2013/22, kwenda kwa
Mkurugenzi wa Ramani wa Wizara ya
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi ikiwataarifu kufufuliwa kwa
barabara hiyo.
Barua hiyo ilikitaka kiwanja namba
10/211 Becon YP 366, 362, 849, 847,
kuacha eneo la barabara kwa ajili ya
jamii.

KURA ZA HAPANA ZAENDELEA KURINDIMA BUNGENI

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba,
akipiga kura wakati wa zoezi la
kupigia kura Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa na bunge hilo mjini
Dodoma jana.Picha/ Khalfan Said.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,
jana walianza kupiga kura kupitisha
Rasimu ya Katiba inayopendekezwa,
huku ikifanyika kampeni kali kusaka
theluthi mbili za wajumbe baada ya
suala la Mahakama ya Kadhi
kushindikana kuingizwa kwenye
rasimu hiyo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
wajumbe watatu wanaowakilisha
madherhebu ya dini na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge,
walipewa fursa ya kuzungumza na
kutoa kauli za kuwashawishi wajumbe
wakubali kuipitisha rasimu hiyo huku
suala kubwa likiwa ni Mahakama ya
Kadhi.
KAULI YA PINDA
Kabla ya hatua ya kupiga kura kuanza
jana alasiri, Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, alilazimika kutoa tamko la
serikali kufuatia taarifa kwamba
wajumbe hususan ambao ni waumini
wa dini ya Kiislamu, wamedhamiria
kuipigia kura ya `Hapana' rasimu
hiyo.
Msimamo wa kuipigia kura za
`hapana' rasimu hiyo ulitolewa
mwishoni mwa wiki na baadhi ya
wajumbe kwa nyakati tofauti bungeni
wakati wakihakiki Rasimu ya Tatu
iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge,
ambayo haijaingiza suala la
Mahakama ya Kadhi kama ambavyo
walitaka iwe.
Akitoa tamko hilo, Waziri Mkuu Pinda,
alisema linafuatia kikao cha
maridhiano cha pamoja kati yake na
Kamati ya Uongozi wa BMK ambacho
pia kiliwashirikisha pia viongozi wa
dini za Kiislamu na Kikristo.
Alisema suala la Mahakama ya Kadhi
ambalo lilianza tangu mwaka 2005,
lilifikia hatua nzuri kwa waumini wa
dini ya kiislamu kuanzisha mahakama
hizo mikoa yote nchini, mwaka
2011/12.
Hata hivyo, alisema tatizo ambalo
limejitokeza kwa sasa ni utekelezaji
wa maamuzi yanayofikiwa kwenye
mahakama hizo kwa upande wa
serikali.
Alisema: “Taifa hili ukiondoa ubaguzi
serikali na kama nchi tumejitahidi
sana kama serikali, tumejitahidi sana
kama nchi kutenganisha shughuli za
imani za dini na shughuli za serikali.”
Alisema huo ndiyo msingi muhimu
sana kwa sababu serikali haina
dini.“Serikali hii haina dini…nchi hii
haina dini, lakini kwa Mtanzania
mmoja mmoja, lazima tuheshimu sana
yale ambayo yeye anaamini kwa imani
yake,” alisema. Alisema kazi ya
serikali ni kuweka mazingira mazuri
ya kuhakikisha kila mmoja anapata
fursa nzuri ya kuamini imani yake.
Alisema nguzo hii muhimu imesaidia
sana kujenga umoja, amani, utulivu
na mshikamano wa taifa hili kwa
kipindi chote hicho na kwamba ni
matarajio ya Katiba mpya nayo italeta
mshikamano huo kwa miaka mingi
ijayo.
“Nawaombeni sana wote katika jambo
hili tusitetereke, tukatae hisia zozote
ambazo zitatuletea uvunjifu wa
amani,” alisema.Alisema baada ya
kikao chao cha Jumamosi, viongozi
hao wa dini waliitaka serikali kutoa
ahadi ni lini sasa wataboresha sheria
zake ili maamuzi yanayotolewa na
mahakama hizo yasiendelee
kupuuzwa yanapopelekwa serikalini.
Pinda alisema kwa kuzingatia
umuhimu huo, serikali itaziangalia
sheria zake mbili ambazo ni Sheria ya
Mahakama ya Mahakimu, Sura yua 11
na Sheria ya Kiislamu, sura ya 375, na
wataleta muswada bungeni ifikapo
Januari mwakani.
Alisema kabla ya kuwasilisha
muswada huo utawashirikisha wadau
wengi na ukifikishwa bungeni
wataangalia namna gani bora ya
kutekeleza maamuzi yao. Anasema
awali alikuwa mbumbumbu sana
katika eneo hilo, lakini baada ya
mazungumzo hayo ameelewa vizuri.
SHEIKH THABIT JONGO
Akizungumza baadaye Mjumbe wa
BMK, ambaye anatoka kundi la 201
(dini), Sheikh Thabit Jongo, alisema
wajumbe bungeni humo wanashukuru
kwa tamko lililotolewa na serikali
kupitia Waziri Mkuu.
“Wajumbe humu ndani wathamini
kauli ile iliyotolewa na Waziri Mkuu…
kitu nyeti na kinachoweza kuvuruga
amani ni suala la imani ya dini mtu.
Humu ndani suala la Mahakama ya
Kadhi lilitaka kutuvuruga,” alisema.
Alisema wapo Waislamu ambao
walikuwa hawaipendi mahakama hiyo
na wapo Wakristo pia ambao hawataki
mahakama hiyo.Lakini kutokana na
tamko lililotolewa na Waziri Mkuu
jana, anawaomba wale wote
waliokuwa na mipango ya kuipigia
kura ya hapana rasimu hiyo sasa
mipango hiyo waifute.
Sheikh Thabit alisema maadui wa
bunge hilo ni watatu ambao ni
kwanza kundi la Umoja wa Katiba ya
Tanzania (Ukawa) ambao wangependa
bunge hilo livunjike.
Alimtaja adui wa pili kuwa ni
aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba, ambaye mara kwa mara
amesikika akilipinga bunge hilo na
hata kudai kuwa atakwenda mitaani.
Adui wa tatu kwa mujibu wa Sheikh
Thabit, ilikuwa ni suala la Mahakama
ya Kadhi, lakini kutokana na tamko la
serikali jambo hilo litashughulikiwa
ifikapo Januari mwakani kwa maana
ya kurekebisha sheria ili utekelezaji
wa maamuzi ya mahakama hizo
yaweze kushughulikiwa na serikali.
Sheikh Hamid Jongo
Kwa upande wake, Sheikh Hamid
Masoud Jongo, alisema kwa kuwa
tamko hilo limetolewa na ofisi ya
Waziri Mkuu kwa maana ya taasisi
basi utekelezaji wake usiwe na
kigugumizi tena kesho kutwa.
Alisema Waislamu hawana nia haswa
ya kuvuruga mchakato huo, lakini
akataka ahadi iliyotolewa na Waziri
Mkuu iheshimiwe.
ASKOFU MTETEMELA
Naye Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa
la Anglikana Tanzania, Donald
Mtetemala, alisema suala la
Mahakama ya Kadhi kwa muda mrefu
lilileta wasiwasi kutokana na hofu ya
kusababisha mpasuko kwa jamii ya
Watanzania.
Alisema upo mpasuko wa kisiasa,
lakini mpasuko wa kidini ni mbaya
sana, hivyo ndiyo maana suala hilo
limechukua muda mrefu ili kulipatia
ufumbuzi.
“Nimeona roho ya kuvumiliana,
ukomavu katika tamko la Waziri Mkuu
Pinda. Alisema rasimu hiyo ina suala
la msingi kwamba serikali na nchi hii
kwa ujumla haina dini.Aliwaomba
waumini wa dini ya Kikristo kuelewa
suala hilo kwa mapana yake.
CHENGE
Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya
Uandishi, Andrew Chenge,
akiwasilisha marekebisho ya Rasimu
ya Katiba inayopendekezwa alisema
rasimu hiyo imefuta na kuandika upya
Ibara ya 2(2) ambayo sasa itakuwa
ikisomeka kuwa, “Rais wa Jamhuri ya
Muungano atakuwa na mamlaka ya
kuigawa Jamhuri katika mikoa, wilaya
na maeneo mengine:
Alisema: “Isipokuwa kwa upande wa
Tanzania Bara, Rais atashauriana na
Rais wa Zanzibar kabla ya kuigawa
Tanzania Zanzibar katika mikoa,
wilaya au maeneo mengine.”
Kabla ya marekebisho hayo, rasimu
yake aliyoiwasilisha wiki iliyopita,
ilisema kwamba Rais wa Jamhuri
angekuwa na mamlaka ya kuigawa
mikoa, wilaya Tanzania Zanzibar,
lakini bila kushauriana na Rais wa
Zanzibar.
Aidha, alitaja marekebisho mengine
kuwa ni kuongeza Ibara mpya ya 44A
inayozungumzia Haki za wakulima,
wafugaji, wavuvi na wachimbaji
madini.
Pia, alisema rasimu imeongeza Ibara
mpya 48A kuhusu Haki ya afya na
maji safi na salama na Ibara ya 55
imefanyiwa marekebisho na kuweka
haki kwa wazee.Alisema Ibara
nyingine iliyoongezwa ni ya 100A
inayohusu Makamu wa Kwanza wa
Rais kushindwa kumudu majukumu
yake.
Kuhusu idadi ya mawaziri alisema
rasimu imeweka ukomo kwamba sasa
imeweka idadi ya mawaziri na
manaibu wao wasizidi 40.
Alisema rasimu pia imeunda Tume ya
Uratibu na Uhusiano ya Muungano
ambayo itakuwa ikishughulika na
usuluhishi wa migogoro kati ya pande
mbili za Muungano kabla ya kufikisha
migogoro hiyo Mahakama ya Juu.
Ibara nyingine mpya ni 208A ambaye
inazungumzia Tume za Kisekta
ambayo itakuwa na tume mbalimbali
za huduma. Kadhalika, alisema
rasimu imeongeza ibara nyingine
mpya 242 kuhusu Udhibiti wa rushwa.
UPIGAJI WA KURA
Zoezi la upigaji kura lilianza kwa
kusuasua baada ya baadhi ya
wajumbe hasa wa kutokea upande wa
Zanzibar, kuikataa kwa kupiga kura za
wazi.
Hatua ya baadhi ya wajumbe kutoka
Zanzibar kupiga kura ya hapana,
ilitarajiwa kutokana na msimamo wao
wa awali waliouonyesha baada ya
suala la Mahakama ya Kadhi
kutoingizwa kwenye Rasimu hiyo.
Wajumbe hao bila woga walipiga kura
ya wazi na kutamka kuwa hawaungi
mkono ibara zote za Rasimu hiyo.
Hata hivyo, wapo baadhi ya

Saturday, September 27, 2014

HUNA HAJA YA KURUDIA RUDIA WIMBO MPYA WA CHRISS BROWN (NEW FLAMES)..LYRICS ZAKE HIZI HAPA

There can be one only you
And, baby, God can never make two
And I know you came here with your
crew
But I promise you that it feels like it's
just us two, aha.
[Bridge: Chris Brown:]
Oh, I don't know what you had
planned to do tonight
But I just wanna be the one to do
you right, right
And we're standing here looking at
each other, baby, eye to eye
And I'm hoping that you're thinking
about leaving with me tonight
[Hook: Chris Brown:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
Try a new thing
And let's spark a new flame
[Verse 2: Usher:]
I can't believe you came here all
alone, baby girl, where's your lover?
Oh, it don't really matter 'cause I got
plans to get to know you better,
yeah.
Baby, baby, baby, baby, let's make
what we got here last forever
Girl, 'cause I don't wanna let you go,
never
[Bridge:]
Oh, I don't know what you had
planned to do tonight
Girl, I just wanna be the one to do
you right, right
And we're standing here looking at
each other, baby, eye to eye
Baby, I hope that you're thinking
about leaving with me tonight
[Hook:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my, baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
Try a new thing
And let's spark a new flame
[Verse 3: Rick Ross:]
Home plate, world series, our nigga
sliding in her
Baby, I'm a boss, I'm talking George
Steinbrenner
Panamera, Yogi Berra, my two-seater
Derek Jeter
Got more stripes than all these niggas
Babe Ruth balling in a Beamer
Collar on my Polo, kisses on my
necklace
All my diamonds watching, now my
watches getting jealous
Smoking on a bomb in my autograph
Lebron's
Yeah, she told me I'm the one, that's
when I only hit it once
[Hook: Chris Brown:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my, baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it

COUNTINHO,JERRY TEGETE KUONGOZA KESHO

Mbrazili Coutinho na Jerry Tegete
watakuwa miongoni mwa wachezaji
wa Yanga watakaoanza pambano la
kesho la ligi kuu ya Bara dhidi ya
Prisons, kwenye Uwanja wa Taifa,
kocha Marcio Maximo amesema.
Akizungumza na Nipashe jana,
Maximo alisema anataraji wachezaji
hao wataleta mabadiliko ya kiuchezaji
Yanga na kupata ushindi baada ya
kuanza kwa kufungwa na Mtibwa
Sugar wiki iliyopita.
"Nimefanyia kazi mapungufu
niliyoyaona (katika mchezo wa
kwanza) lakini furaha yangu ni
kurejea kwa washambuliaji Tegete na
Coutinho ambao naamini wataongeza
nguvu na kutuletea ushindi kwenye
mchezo wa Jumapili (kesho),"
alisema Maximo.
Uwepo wa Coutinho, Tegete na
Mbrazili mwingine 'Jaja' kwenye safu
ya ushambuliaji na kucheza kwenye
Uwanja wa Taifa kunampa Maximo
moyo wa kuibuka na ushindi wake wa
kwanza nchini kama kocha wa klabu
ya ligi kuu ya Bara.
Maximo ambaye alikuwa mwalimu wa
Taifa Stars kwa miaka minne tangu
mwaka 2006, amesema beki wa
kushoto Oscar Joshua aliyeumia
kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa na
mshambuliaji Hussein Javu
hawatacheza.
Wote wanauguza maumivu ya nyama
za paja.
"Wachezaji wengine wote wapo katika
hali nzuri na naamini wataniletea
ushindi."
Kukosekana kwa Joshua kunatarajiwa
kumfanya Maximo amrudishe Mbuyi
Twite kucheza beki ya kushoto.
Maximo ambaye pamoja na timu yake
wanapewa nafasi kubwa zaidi ya
kutwaa ubingwa wa Bara msimu huu,
alishindwa kuzuia mwendelezo wa
rekodi mbaya dhidi ya Mtibwa kwenye
uwanja wa Jamhuri kwa miaka ya
karibuni timu yake ilipofungwa 2-0.

PATA BRAND NEW VIDEO YA CHRISS BROWN FT. RICK ROSSAY &USHER RAYMOND

DOWNLOAD VIDEO

KAMA HUJAIPATA AUDIO TRACK MPYA YA MAVOCKO PACHA WANGU...DOWNLOAD HAPA

DOWNLOAD

Thursday, September 25, 2014

NEW TRACK: MKUBWA NA WANAWE-MSAMAHA

BOFYA HAPA KUI DOWNLOAD

BRAND NEW TRACK BY MKUBWA NA WANAWE-BORA KIJIJINI

DOWNLOAD

BRAND NEW VIDEO BY RICH MAVOCKO-PACHA WANGU

MSANII ALIEKUA KIMYA KWA MUDA MREFU KIDOGO BAADA YA KUACHIA WIMBO WAKE WA ROHO YANGU SASA ADONDOKA NA TRACK NYINGINE INAYOENDA KWA JINA LA PACHA WANGU

   BOFYA HAPA KUICHEK NA KU DOWNLOAD

PATA LYRICS ZA NYIMBO MBALIMBALI KUANZIA SASA TUNAANZA NA WIMBO WA TYGA-FADED

Faded"
(feat. Lil Wayne)
(Intro)
I don't give a fuck
{Tyga tyga tyga nice to see you}
[Tyga]
Young Nino, fuck a bitch in a pea
coat
Carlito, Scarface, AL Pacino
Bun B do, Pimp C, R-PIDO though
I goes deep in that pussy, Dan
Marino
She wanna be the one, fuck her to my
own single
Break a bitch heart, no future miss
cleo
Snap back, au-au-automatic reload
Flyer than a fucking beatle, you can't
beat 'em
Vampire fuck up your evening
I pop up and eat lunch, leave you in
the cement
Don't believe it, stripe like a fucking
Adidas
The gun selena, give a nigga bieber
fever
Real fucking hot, put it in park
Take a shot, higher than a tube sock
You a bop, give me top top, as I load
the guap
Man these niggas say I'm fly but to
her I'm god
[Hook]
I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
[Tyga]
Fuck is up, nigga's stomping in my
chucks
Yeah, I make it rain, dear, cause I'm
all about my bucks
Use the butt I'm in the front, dick up
in her cunt
And I put it in her hole, hole in one,
putt putt (wahhhhhh)
Super McNasty, why you McLoving
When the bitch call me daddy
Pimp no caddy, she wish she never
had me
Treat her like a dog, called the bitch
lassy
Young savvy, bang her like Cincinnati
Above average, fly like I'm Aladdin
They bend backwards, throw the
pussy at them
I'm Ben Wallace, dunk up in your
basket
Balls in the air, no games,
I'm serious, double dare
There's too many bitches,
Why these niggas wanna stare
Patron up in here
Nigga this ain't no beer
[Hook]
I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
[Lil' Wayne]
Mama, there go that monster
Abracadabra, magic Johnson
My motherfucking doctor
Said I need a doctor
So I called house,
Now I am a pill popper
Faded like skinnys
Young money we winning
I told her if I change
She won't get a penny
Milking that shit, pregnant bitch
titties
Bringing home the bacon
I'm fucking miss piggy
Loaded like a semi, semi-naked
pictures
She knows my dick, she call it nigga
Richard
Prior to me cummin, I had to stick my
thumb in
Her ass one time, smell my finger
make you vomit
Flyer than a hornet, the shoe fit I
worn it
She tried to jack me off, can't beat it,
join it
Tunechi, coochie that what she call
it,
Flag Scarlett, I killed it, mourn it
[Hook]
Faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
[Lil Wayne:] Young Moolah baby!
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck

WASANII WAHAMASISHWA KUSHIRIKI KWENYE SIKU YA SANAA

Viongozi wa mashirikisho ya filamu
na sanaa za ufundi wamewataka
wasanii wa fani mbalimbali kujitokeza
katika kushiriki semina
zitakazoendeshwa katika Siku ya
Msanii Tanzania.
Semina ya Siku ya Msanii inatarajiwa
kufanyika Oktoba 22 na 23 mwaka huu
katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere
(Makumbusho Posta) na wasanii
watafundishwa mambo
mbalimbali.Rais wa Shirikisho la
Sanaa za Ufundi, Adrian Nyangamale,
alisema wasanii wanapaswa
kujiandikisha kwenye semina hizo ili
kupata ujuzi wa mambo mbalimbali.
“Semina hizi ni muhimu kwa sababu
kutakuwa na wataalamu kutoka katika
sekta mbalimbali ambao watakuja
kutoa mafunzo kwenye semina hizo,
jambo ambalo litachangia uelewa na
elimu ya wasanii, tumekuwa
tukilalamika kuwa hatupati fursa za
elimu lakini Siku ya Msanii imetupa
hiyo nafasi sasa tuitumie,” alisema.
Naye Makamu wa Rais wa Shirikisho
la Filamu, Selemani Ling’ande alisema
wasanii wajitokeze kwenye semina
hizo lakini pia aliwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi katika kupiga
kura za kupata watu watakaowania
tuzo za Siku ya Msanii.
“Semina ni muhimu lakini kuna suala
la kutambulika mchango wa wasanii,
hapa ndiyo Watanzania
wanapotakiwa kufanya mapendekezo
yao, kuna fomu zinatolewa kwenye
magazeti na mitandao juu ya Tuzo za
Humanitarian Award na Life Time
Achievement ambazo wasanii wote
wanaweza kushindanishwa,” alisema.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya
Haak Neel Production, Godfrey Katula,
ambaye kampuni yake ndiyo imepewa
jukumu la kusimamia Siku ya Msanii,
alisema Watanzania wajitokeze
kupendekeza majina ya wasanii
wanaostahili kupata tuzo na Kamati
ya Utafiti itakwenda kuhakiki taarifa
zote zilizowasilishwa kwao.
“Kazi za wasanii zinaanza
kutambulika hapo, wananchi
wanawajua hivyo ni fursa yao
kuonyesha kuthamini kazi zao, lakini
pia tunawataka wasanii wajitokeze
kwenye semina ambazo zitafanyika
kwa siku mbili ili kupata elimu
sahihi,” alisema.
Siku ya Msanii inaandaliwa na
Kampuni ya Haak Neel Production
kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa
la Taifa (BASATA).

CHADEMA NA POLISI WAENDELEA KUZOZANA

Jeshi la Polisi limeendelea
kusuguana na Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) wakati
wafuasi wa chama hicho wakitaka
kuandamana huku polisi
wakiwadhibiti.
Mkoani Kagera, Jeshi la Polisi
limepanga askari wake kila mtaa
katika manispaa ya Bukoba kwa lengo
la kudhibiti maandamano hayo.
Kaimu Kamanda wa polisi mkoani
Kagera, Gilles Muroto, alisema
kupangwa kwa askari hao
kumetokana na kutoeleweka
maandamano ya wafuasi wa chama
hicho yataanzia katika mtaa upi.
“Tunafahamu siku ya kwanza tutapata
changamoto kutokana na askari
wengi kupangwa kudhibiti
maandamano hayo, lakini kadri
tunavyoendelea tutajipanga vizuri
hakuna shughuli ya kuhudumia
wananchi itakayokwama,” alisema
Muroto.
Alisema kuwa Septemba 22 mwaka
huu walipokea barua ya Chadema
wakiomba kuandamana kesho yake
kuanzia saa 3:00 asubuhi, lakini
maombi hayo hayakukubaliwa
kutokana na kupigwa marufuku na
makao makuu ya jeshi hilo.
Jijini Dar es Salaam, jana polisi
walizizingira ofisi za Chadema makao
makuu kudhibiti wafuasi wa chama
hicho wasiandamane.Askari hao
wakiwamo wa Kikosi cha Kutuliza
Ghasia (FFU), walikuwa katika doria
wakiwa kwenye magari mawili aina ya
Land Rover pamoja na silaha za moto.
Hali hiyo iliwafanya wafuasi wa
Chadema kukaa katika vikundi
wakijadili hali ilivyo katika maeneo ya
kuingilia katika makao makuu ya
chama hicho.Afisa Habari wa
Chadema, Tumaini Makene alisema
wanalishukuru jeshi hilo kwa
kuwasaidia kuandamana katika
maeneo mbalimbali ya nchi.
Aliongeza kuwa wana njia 198 za
kuandamana ikiwa ni pamoja na
kuwatumia ujumbe mfupi viongozi wa
Bunge Maalumu la Katiba kuwaeleza
kuwa hatufurahishwi na
kinachoendelea bungeni.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es
Salaam, Suleman Kova, alisema
wamejipanga kudhibiti fujo
zitakazotokea. Jijini Mwanza,
Mwenyekiti wa Chadema wa mkoa wa
mwanza, Adrian Tizeba, jana alitiwa
mbaroni na Polisi, baada ya kufanya
mkutano wa waandishi wa habari
kuzungumzia maandamano.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo,
Valentino Kilowoko, alithibitisha
kukamatwa kwa Tizeba na kusema
walikuwa wanaendelea kumhoji.
Kabla ya kukamatwa, Tizeba alilitaka
Jeshi la Polisi mkoani humo
kushirikiana nao katika maandamano
ya amani yatakayofanyika leo kupinga
Bunge la Katiba linaloendelea mjini
Dodoma.
Alisema licha ya polisi wilaya zote za
mkoa wa Mwanza kukataa barua za
taarifa za kuwapo maandamano hayo,
lakini wamekusudia kuandamana na
kuwaomba polisi nao washiriki.
“Haya ni maandamano ya amani,
tunaomba hata polisi washiriki nasi
kesho (leo) ili kufikisha ujumbe wa
matumizi mabaya ya pesa za umma
katika bunge hilo linaloendelea
Dodoma hivi sasa,” alisema Tizeba.

ZITTO KABWE KUWAPATANISHA DIAMOND NA ALI KIBA

Mbunge wa Kigoma Kaskazini
(Chadema), Zitto Kabwe, amejitosa
kusuluhisha ugomvi wa muda mrefu
wa wasanii wawili wa muziki wa
kizazi kipya nchini, Ali Kiba na
Nasibu Abdul 'Diamond'.
Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati
akihojiwa katika Kipindi cha Mkasi
kinachorushwa na Kituo cha
Televisheni cha EATV baada ya
kuulizwa kuwa ni jitihada gani
amezifanya kusuluhisha ugomvi wa
wasanii hao akiwa kama mlezi wa
wasanii wanaotoka mkoani Kigoma.
Alisema anafahamu kuwapo kwa
ugomvi wa kutoelewana kati ya
wasanii Ali Kiba na Diamond na
kwamba alishawahi kufanya jitihada
za kuwaita kila mmoja kwa nyakati
tofauti.
Alifafanua kuwa katika kuhakikisha
anawasuluhisha wasanii hao,
anaifanya kazi hiyo kwa umakini kwa
sababu hataki kuonekana anaingilia
maisha ya watu na kwamba ana imani
atafanikiwa kuwapatanisha.
Kuhusu madai kwamba ana uhusiano
wa kimapenzi na msanii Mwasiti
Almas, alisema ni kweli kumekuwapo
na uvumi huo lakini kimsingi hana
uhusiano wowote wa kimapenzi na
msanii huyo.
"Nasikitishwa na madai hayo
yanayotolewa na baadhi ya watu,
Mwasiti ni kama dada yangu ambaye
nimekuwa nikimsaidia katika kazi
zake, kuhusishwa naye kimapenzi ni
jambo linalonisononesha,"alisema.
Zitto alisema wanaomhusisha katika
suala la mapenzi na msanii huyo ni
kwa sababu Mwasiti ameimba wimbo
ambao amemtaja yeye (Zitto) lakini
kiukweli hana uhusiani naye wa
kimapenzi.
Alipoulizwa ni lini ataoa, alisema
bado 'yupo yupo' na kwamba kuna
mwanamke aliyemtaja kwa jina la
Jack ambaye amezaa naye mtoto
ambaye kwa sasa miaka nane na
anasoma darasa la pili nchini Uganda.
KAMPUNI YA LEKA DUTIGITE
Kuhusu Leka Dutigite inayounganisha
wasanii wa Kigoma All Stars, alisema
ni kampuni ambayo kila msanii
anayetoka mkoani Kigoma ana hisa
na ikipata faida wanagawana.
Zitto alisema Leka Dutigite pia
inamiliki kampuni nyingine ambayo
imekuwa ikipata kazi mfano katika
Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na
yeye kama mlezi amekuwa akitoa
fedha zake kusaidia.

WAREMBO WA MISS TANZANIA WATALII MTO WA MBU

Warembo wanaotarajia kushiriki
shindano la urembo la taifa mwaka
huu "Redd's Miss Tanzania 2014" leo
wanatarajia kutembelea eneo la Mto
wa Mbu kushuhudia maajabu yaliyoko
kwenye mto huo ulioko Karatu
mkoani Arusha ikiwa ni sehemu ya
kufanya utalii wa ndani
Akizungumza na gazeti hili jana kwa
njia ya simu, Ofisa Habari wa Kamati
ya Miss Tanzania, Haidan Rico,
alisema kuwa wakiwa eneo hilo,
warembo walipewa maelezo muhimu
kuhusiana na mto huo na dhumuni la
kuwatembeza warembo hao katika
vivutio mbalimbali ni kutaka
kushawishi jamii kufanya utalii
Rico alisema kuwa wanaamini
warembo hao watafikisha ujumbe
katika familia zao na kubadili mawazo
kwamba utalii ni kwa ajili ya wageni
pekee.
Alisema kuwa kesho Jumanne
warembo hao wataelekea Ngorongoro
Crater kuona jinsi eneo hilo
lilivyobonyea kufuatia mlipuko wa
volkano.
Alisema kuwa tayari warembo hao
wameshatembelea katika lango la
kupanda mlima Kilimanjaro na
kuelezwa mazingira yanayozunguka
eneo hilo, Tarangire na kufanya kazi
za kijamii kwenye hospitali za Kilema
na Marangu ambapo walitoa misaada
ya sabuni, vyandarua, dawa ya meno,
miswaki na mafuta ya kujipaka kwa
watoto na wanawake waliolazwa
kwenye hospitali hizo.
Pia washiriki hao walitembelea
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (KIA) na wakiwa hapo
walijifunza mbinu ambazo askari
wanatumia kukagua abiria ambao
wanasafiri na bidhaa zisizoruhusiwa
kama vile dawa za kulevya.
Pia alisema washiriki watamtembelea
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini na
baadaye Hifadhi ya Mbuga ya Arusha.
Warembo hao 30 kutoka mikoa
mbalimbali nchini ambao wako katika
ziara hiyo ni pamoja na Dorice Mollel,
Sofia Masey, Lilian Timothy, Junes
Ndalima, Maureen Godfrey, Martha
John, Naba Magambo, Raisa Julius,
Happiness Samuel, Evelyn Baasa,
Lilian Kamazima, Elizabeth Tarimo,
Nidah Katunzi, Lucy Diu, Mariam
Hussein, Maria Shilla, Camilla John,
Queen Latifa Hashim na Dorren Beno.
Warembo wengine ni Sitti Mtemvu,
Salama Saleh, Patricia Pontain,
Rachel Clavery, Mary Emmanuel,
Nicole Sarakikya, Dorren Robert,
Jihan Dimachk, Nasreen Abdul,
Sabina Thomas na Happinness
Sosthenes.
Happiness Watimanywa kutoka
mkoani Dodoma ndiye mrembo
anayeshikilia taji hilo la taifa na
baadaye mwaka huu ataiwakilisha
nchi kwenye fainali za urembo za
dunia.

TANZANIA YASHUKA VIWANGO FIFA

Tanzania imeporomoka tena kwenye
viwango vya soka vinavyotolewa kila
mwezi na Shirikisho la Soka la
Kimataifa (Fifa), baada ya kuanguka
kwa nafasi tano katika viwango
vilivyotolewa jana.
Tanzania, ambayo ilifungwa 2-0 na
Burundi katika mechi ya kimataifa ya
kirafiki iliyopita, sasa inakamata
nafasi ya 115 duniani na 33 barani
Afrika ikiwa nyuma ya Uganda
wanaoongoza Afrika Mashariki
wakiwa nafasi ya 79 duniani na 19
Afrika, Rwanda walioko nafasi ya 93
duniani na 25 Afrika na Kenya
walioporomoka kwa nafasi saba
wakiwa nafasi ya 30 Afrika na 111
duniani.
Aligeria waliopanda kwa nafasi nne,
wanaongoza barani Afrika wakiwa
nafasi ya 20 duniani wakifuatwa na
Ivory Coast walioshuka kwa nafasi
tatu baada ya kukubali kichapo cha
mabao 4-1 kutoka kwa Cameroon
waliopanda kwa nafasi 12 na
kukamata nafasi ya nane Afrika na 42
duniani.
Nafasi ya tatu barani Afrika inakaliwa
na Tunisia (31) wakipanda kwa nafasi
11 wakifuatwa na Ghana (33), Senegal
(36), Nigeria (37) na Cape Verde (41).
Guinea waliopanda kwa nafasi 16
wanakamata nafasi ya tisa barani
Afrika na 48 duniani huku Burkina
Faso waliopanda kwa nafasi 10
wakifunga pazia la 10 bora barani
Afrika wakifungana na Guinea katika
nafasi ya 48 duniani.
Uganda pia ni wa kwanza katika
Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki
na Kati wakifuatwa na Rwanda,
Kenya, Tanzania, Burundi, Ethiopia
(39, 132), Sudan (40, 133), Shelisheli
(47, 172), Sudan Kusini (50, 185),
Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204)
huku Djibouti wakifunga mlango
Cecafa na Afrika wakiwa 54 Afrika na
205 duniani.
Mabingwa wa dunia, Ujerumani
wanaongoza 10 bora ulimwenguni
wakifuatwa na Argentina, Colombia
waliopanda kwa nafasi moja
wakiwashusha Uholanzi, Ubelgiji,
Brazil, Uruguay, Hispania, Ufaransa
na Uswis.

Wednesday, September 24, 2014

OKWI ADAI KUA YANGA WATATULIA TU

Licha ya kupika mabao yote ya Simba
katika mechi yao ya kwanza ya Ligi
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL)
msimu huu waliyotoka 2-2 dhidi ya
Coastal Union kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam juzi,
mshambuliaji Emmanuel Okwi
amesema hakuwa katika kiwango
chake.
Okwi, aliyejiunga na Simba dakika za
mwisho kabla ya kufungwa kwa
dirisha la usajili msimu huu akitoka
Yanga, alisababisha mabao yote ya
Simba juzi licha ya mashabiki wa
Yanga kumzomea mwanzo mwisho
jambo analoamini muda si mrefu
watatulia baada ya kurejea katika
makali yake.
Bao la kwanza la Simba lilipatikana
baada ya Okwi kukwatuliwa nje ya
mstari wa eneo la hatari la Coastal
Union, hivyo adhabu hiyo kuzaa
matunda kupitia kwa mpigaji Shabani
Kisiga kabla ya Mganda huyo tena
kutoa pasi ya mwisho ya bao la pili
kwa mfungaji bora wa VPL msimu
uliopita, Mrundi Amissi Tambwe.
Kisiga alifunga kwa 'frikiki'
iliyomshinda kipa wa Coastal, Shaban
Kado wakati mabao ya mabingwa hao
wa Tanzania Bara 1988 yalifungwa na
mtokea benchi Lutimba Yayo na
mshmbauliaji wa zamani wa Gor
Mahia ya Ligi Kuu ya Kenya, Rama
Salim.
Mara tu baada ya mechi hiyo
iliyochezeshwa na refa Jacob Adongo
kutoka Mara kumalizika, Okwi
aliliambia NIPASHE kuwa bado
hajafikia katika kiwango chake cha
kusakata soka.
“Mara nyingi sipendi kuzungumzia
kiwango changu binafsi kuliko cha
timu, tulicheza vizuri kipindi cha
kwanza na Coastal walicheza vizuri
kipindi cha pili,” alisema Okwi.
“Sijafurahishwa sana na kiwango
nilichoonyesha leo (juzi), nitajitahidi
kuongeza mazoezi ili mechi ijayo
niisaidie timu yangu kupata ushindi,”
alisema zaidi Mganda huyo ambaye
muda wote wa mechi ya juzi alikuwa
akizomewa na mashabiki wa Yanga
waliokuwa wameingia uwanjani
kutazama mechi hiyo.
Alipoulizwa juu ya zomea zomea
inayofanywa na mashabiki wa Yanga
dhidi yake, Okwi alisema: “Sina muda
nao, mimi nimeshakuwa mchezaji
halali wa Simba, mambo yote
kuhusiana na Yanga hayanihusu.
Ninaamini nitakapokuwa katika
kiwango changu, hawatanizomea
tena,” alisema.
Okwi, mchezaji wa zamani wa SC Villa
ya Ligi Kuu ya Uganda na Etoile du
Sahel ya Tunisia, amejiunga na Simba
baada ya uongozi wa Yanga
kuwasilisha nyaraka katika Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF) zikionyesha
kuwa mkataba wake wa miaka miwili
na nusu na klabu hiyo ya Jangwani
aliousaini Desemba 13, mwaka jana,
umevunjwa.

MAGOLI 18 LIGI KUU YASHINDWA KUVUJA REKODI

Magoli 18 yamefungwa kwenye mechi
saba za ufunguzi wa Ligi Kuu
Tanzania Bara iliyoanza Jumamosi
iliyopita, lakini yameshindwa kuvunja
rekodi ya magoli ya msimu uliopita.
Kwenye mechi za ufunguzi wa Ligi
Kuu msimu uliopita jumla ya magoli
19 yalipatikana.
Ligi ya msimu huu imeanza kwa Azam
FC kuitandika Polisi ya Morogoro
mabao 3-1, Mtibwa Sugar kuichapa
Yanga mabao 2-0, Stand United ya
kutandikwa nyumbani mabao 4-1
dhidi ya Ndanda FC kutoka Mtwara,
wakati Mgambo JKT ya Tanga
iliifunga Kagera Sugar bao 1-0.
Mechi nyingine ilikuwa ni Ruvu
Shooting kupata kipigo nyumbani cha
mabao 2-0 kutoka kwa Prisons ya
Mbeya, Mbeya City kulazimishwa sare
ya bila kufungana dhidi ya JKT Ruvu,
huku Simba ikibanwa mbavu katika
sare ya 2-2 dhidi ya Coastal Union,
hivyo kuzaa mabao 18.
Magoli 19 ya mechi ya ufunguzi
msimu uliopita kwa mujibu wa
kumbukumbu zetu yalipatikana kwa
Yanga kuinyuka Ashanti mabao 5-1,
Mtibwa kutoka sare ya bao 1-1 dhidi
ya Azam, JKT Oljoro ikainyuka
Coastal Union mabao 2-0, Mgambo
ikachapwa 2-0 dhidi ya JKT Ruvu,
Simba ikatoka sare ya mabao 2-2
dhidi ya Rhino ya Tabora, Mbeya City
ikatoka sare ya bila kufungana dhidi
ya Kagera Sugar na Ruvu Shooting
ikaitandaika Prisons mabao 3-0.
Katika hatua nyingine, mchezaji wa
Mgambo Shooting Ramadhani Pera
ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa
kwanza kufunga bao kwenye Ligi kuu
alipofunga bao pekee dhidi ya Kagera
Sugar katika dakika ya 12 kwenye
raundi ya kwanza ya ligi hiyo
Jumamosi.
Mabao yote yaliyopatikana kwenye
mechi nyingine yalifungwa baada ya
dakika hizo.
Shaaban Kisiga wa Simba anashikilia
rekodi ya kufunga bao la mapema
zaidi katika dakika ya saba dhidi ya
Coastal katika mechi ya kufunga
raundi ya kwanza Jumapili.

TIKETI ZA KIELEKTRONIKI ZAANZA KUJIBU

Mfumo wa tiketi za elektroniki katika
mechi za soka nchini umeanza kuzaa
matunda baada ya jana Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), kuweka wazi
kwamba mapato ya milangoni
yameongezeka.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana mchana,
Mkurugenzi wa Mashindano wa
shirikisho hilo, Boniface Wambura,
alisema utumiaji wa tiketi za
elektroniki umefanikiwa kudhibiti
hujuma za mapato ya milangoni
kwenye viwanja ambavyo tayari
vimeshasimikwa mfumo huo.
Wambura alisema kwa sasa wanapata
mapato halisi ya mechi husika
kulingana na idadi ya watu waliokata
tiketi.
“Hatutarudi nyuma katika hili,
tutaendelea kutumia tiketi za
elektroniki kwenye viwanja vyote
vilivyosimikwa mfumo huu,” alisema
Wambura na kuongeza: “Kuna viwanja
kama CCM Kirumba jijini Mwanza na
Sheikh Amri Abeid jijini Arusha vina
mfumo huu lakini havitumiwi na timu
za Ligi Kuu.
Tutahakikisha mechi za Ligi Daraja la
Kwanza zinazochezwa kwenye
viwanja hivyo vinatumia tiketi za
elektroniki ili watu waishio katika
majiji hayo pia wauzoee.”
Mkurugenzi huyo alisema watu wote
wanaojaribu kuingia viwanjani kwa
kutumia tiketi feki wamekuwa
wakinaswa kwa kutumia mashine za
utambuzi wa tiketi za elektroniki
(PDA), hivyo kwa sasa hakuna mtu
anayeingia kwenye viwanja vilivyo na
mfumo huo akitumia tiketi bandia.
Akitangaza mapato ya mechi za wiki
iliyopita za Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara (VPL), Wambura
alisema yameongezeka kwa kiasi
kikubwa, sababu kubwa akisema ni
matumizi ya mfumo wa tiketi za
kisasa za kielektroniki.
Wambura alisema mechi ya Mtibwa
Sugar dhidi ya Yanga iliyochezwa
kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini
Morogoro Jumamosi na kumalizika
kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa
mabao 2-0, imeingiza Sh. milioni 59
kutokana na viingilio vya mashabiki
11,499 waliokata tiketi za Sh. 5,000.
Mapato hayo ni ongezeko la Sh.
milioni 12 ikilinganishwa na mapato
ya mechi kati ya timu hizo kwenye
uwanja huo msimu uliopita.
Aidha, Wambura alisema kuwa mechi
ya Simba dhidi ya Coastal Union
iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam Jumapili huku
timu hizo zikitoka sare ya mabao
mawili, imeingiza Sh. milioni 124.7
zilizotokana na viingilio vya
mashabiki 22,114 waliokata tiketi
kuingia kwenye uwanja huo wenye
uwezo wa kuketisha watazamaji
57,558.
Simba na Coastal Union ziliingiza Sh.
milioni 36.8 zilipokutana katika mechi
ya ligi hiyo kwenye uwanja huo
msimu uliopita.
Utumiaji wa tiketi hizo za kielektroniki
ni utekelezaji wa mapendekezo
yaliyomo kwenye ripoti ya Kamati
Maalum ya Kudhibiti na Kuboresha
Mapato ya TFF iliyotolewa 2011 na
agizo la serikali lililotolewa katikati
ya mwaka huu.
Mei 2011 Kamati Maalum ya Kudhibiti
na Kuboresha Mapato ya TFF
iliyoongozwa na Rais Mstaafu wa
shirikisho hilo, Leodegar Tenga, ilitoa
ripoti yenye kurasa 95 ikionesha
uhujumu mkubwa wa mapato
utokanao na matumizi ya tiketi za
kawaida, hivyo kamati ikapendekeza
TFF ianze kutumika tiketi za kisasa za
kielektroniki.
Aidha, Juni mwaka huu, serikali
iliiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) kuiiamuru TFF kutumia mfumo
wa tiketi za kielektroniki kwenye
viwanja mbalimbali vya soka nchini ili
kudhibiti uhujumu wa mapato ya
milangoni.
Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya
Bunge ya Uchumi, Viwanda na
Biashara kuhusu utelezaji wa
majukumu ya Wizara ya Fedha na
Uchumi kwa mwaka wa fedha 2014/15
Bungeni mjini Dodoma Juni 4, mwaka
huu, mwenyekiti wa kamati hiyo,
Luhaga Mpina aliitaka TRA kutoa
sharti kwa TFF kutumia mfumo wa
tiketi za elektroniki ili kuongeza
mapato ya nchi.
"Kamati inashauri TRA iweke sharti la
lazima la kuitaka TFF kutumia mfumo
wa tiketi za kielektroniki katika kuuza
tiketi zake ikiwa ni jitihada za
kuongeza mapato ya serikali," alisema
Mpina.
Mbunge huyo wa Kisesa (CCM),
alisema kwa muda mrefu serikali
imekuwa haipati mapato ya kutosha
kutoka katika sekta ya michezo
hususan mpira wa miguu ulio chini ya
TFF kutokana na mfumo dhaifu wa
ukusanyaji fedha kipindi cha kuuza
tiketi.

KIONGERA KUIKOSA YANGA

Mshambuliaji Paul Kiongera wa
Simba huenda akaikosa mechi ya
kwanza dhidi ya watani wao wa jadi,
Yanga msimu huu wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara itakayopigwa
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam Oktoba 12 baada ya kuumia
goti katika mechi iliyopita.
Kiongera alitokea benchi dakika ya 67
akichukua nafasi ya mfungaji bora wa
msimu uliopita, Mrundi Amissi
Tambwe, lakini dakika mbili kabla ya
mechi hiyo waliyotoka 2-2 dhidi ya
Coastal Union kumalizika, Mkenya
huyo alilazimika kumpisha Amri
Kiemba baada ya kugongana na kipa
Shaaban Kado wa Coastal na kuumia.
Taarifa zilizolifikia NIPASHE jana
kutoka ndani ya uongozi wa Simba
zilieleza kuwa Kiongera ameumia goti
na jana alipelekwa Hospitali ya Taifa
Muhimbili kufanyiwa vipimo.
Mmoja wa viongozi wa Simba (jina
tunalo) alisema mchezaji huyo ana
maumivu sugu ya goti hilo baada ya
kuumia awali akiwa kwao, Kenya.
Kiongozi huyo alisema Kiongera
anaweza kuwa nje ya uwanja kwa
muda wa kati ya wiki sita hadi miezi
miwili kabla ya kuanza mazoezi
mepesi, hivyo hatacheza mechi ya
Oktoba 12 ya watani wa jadi Simba na
Yanga.
Alibainisha kuwa kumeibuka hali ya
wasiwasi ndani ya Simba kwamba
huenda hawakufanya uamuzi sahihi
kumsajili Mkenya huyo kabla ya
kumfanyia vipimo vya afya.
Majeruhi wengine wa Simba ni beki
wa kushoto Issa Rashid ‘Baba Ubaya’
aliyeumia nyama za paja wiki mbili
zilizopita mazoezini, ambaye
inaelezwa kuwa yuko katika wiki ya
mwisho ya mapumziko na winga
Haruna Chanongo aliyeumia goti pia
Jumapili wakati wakichuana na
Coastal. Imeelezewa kuwa Chanongo
atakuwa nje kwa siku nne tangu
kuumia kwake.
Habari njema zaidi kwa Simba kwa
sasa ni kurejea kwa kiungo
mpambanaji Jonas Mkude, ambaye
Daktari wa Simba, Yassin Gembe
amesema anaweza kuanza kucheza
hata Jumamosi dhidi ya Polisi
Morogoro endapo kocha atampanga.
“Ni uamuzi wa kocha tu, lakini ukweli
ni kwamba Mkude yuko fiti kabisa
kwa sasa na anaweza kuanza
kucheza, uzuri ni kwamba pamoja na
kuwa nje kwa muda mrefu, lakini
hajaongezeka uzito,” alisema Gembe.
Mkude hajawahi kuichezea Simba
chini ya kocha aliyerejea kwa mara ya
tatu nchini kuinoa timu hiyo,
Mzambia Patrick Phiri. Katika mechi
iliyopita kiungo Mrwanda Pierre
Kwizera alicheza nafasi ya Mkude
lakini alionekana wazi kutoimudu.
Baada ya Chanongo kuumia, winga
Uhuru Seleman aliingizwa lakini
baada ya mechi kumalizika huku
Coastal wakirudisha mabao yote,
Phiri aliweka wazi kwamba pengo la
Chanongo halikuzibika ipasavyo.
Kikosi cha Simba kilirejea tena
kambini visiwani Zanzibar kujiandaa
kwa mechi yao inayofuata Jumamosi
dhidi ya Polisi Morogoro.